TRIBUTE TO MUAMMAR GADDAFI

Wednesday, February 22, 2012

HEIGHTENING IRANIAN TENSIONS






by Stephen Lendman


For months, Iran faced baseless accusations. They include:


  • the spurious US Saudi ambassador assassination plot;


  • charges about developing nuclear weapons;


  • being the "world's leading state sponsor of terror," according to AIPAC;


  • targeting Israeli officials in India, Georgia, and Thailand; and


  • planning Israeli Defense Minister Ehud Barak's assassination, according to The Israel Project citing Kuwait's Al Jarida newspaper.


All of the above don't pass the smell test. Charges are baseless on their face. Yet major media scoundrels headline them for days. In the process, they heighten tensions for belligerent intervention.


Moreover, they ignore past US/Israeli terrorist attacks blamed on Arabs, and both countries' notorious histories of targeted assassinations and other destabilization schemes.


Former National Security Advisor Zbigniew Brzezinski believes Iran may be blamed for a false flag on US soil to justify war. Former Marine Corps Intelligence/CIA case officer Robert David Steele expressed the same view. So do others to give America and Israel the war they want, no matter the potential catastrophic consequences.


Since the 1980s, Washington planned regime change. Israel offers ready support. As a result, war on Iran's been ongoing by other means.


They include computer viruses and other cyber attacks, other sabotage, multiple rounds of sanctions, attempts to cripple its central bank and oil exports, targeted assassinations, deadly explosions, sophisticated satellite, drone, and other type spying, bogus accusations, imposing a virtual blockade to isolate Tehran, and ongoing saber rattling stopping just short of bombs away.


When Washington's planned regime change train leaves the station, it doesn't stop until mission accomplished by whatever means necessary. Against Syria and especially Iran, it literally risks WW III as Russia and China may intervene to protect their own vital interests.


Provocative Major Media Reports


Inflammatory reports continue. On February 15, The New York Times headlined, "Israeli Envoy Links Bangkok Bombs to Attacks in India and Georgia," saying:


Iranians were detained after "an explosion tore the roof off their rented house...." Despite no credible evidence, they're suspected of targeting Israeli diplomats. According to Thai police chief General Prewpan Dhamapong:


"This much I can tell you - the target of the operation was specifically the Israeli diplomatic staff."


Again, accusations without credible evidence are baseless. With nothing to gain and everything to lose, Iran painstakingly avoids provocations. In contrast, Israel benefits greatly. Moreover, the India/Georgia/Thailand attacks bear classic Mossad fingerprints. Yet no Western reports suggest it.


Instead, fingers point spuriously one way. In Thailand, police discovered explosive devices in the suspect's rented house. They were similar to those used in India, Georgia, and Mossad attacks on Iranian nuclear scientists.


Israel's Thai ambassador Itzhak Shoham called them "connected." Why not as evidence suggests Mossad responsibility, not Iran.


Tehran officials called accusations baseless. Foreign Ministry spokesman Ramin Mehmanparast said "We categorically reject the accusations made by the Zionist regime. They are part of a propaganda war. Iran condemns all acts of terrorism."


He added that Israel blames Iran for its state terrorist acts to incite anti-Iranian sentiment. Multiple Thailand incidents occurred the day after failed bomb attacks targeted Israeli embassy staff in India and Georgia.


Following the Bangkok incidents, Thailand's tourism ministry announced suspension of visas to Iranian citizens. Last year, 148,235 were issued.


On February 16, The Times headlined, "Inquiry Widens on Suspected Iranian Plot on Israel," saying:


Indian and Thai "criminal inquiri(es)" continue. Iran and Hezbollah emphatically denied involvement. In a televised address, Secretary-General Hassan Nasrallah said:


"Regarding the explosions that took place in India, Georgia and Thailand, I can tell you categorically that Hezbollah had nothing to do with them."


Iran was just as emphatic denying what's clearly baseless and part of longstanding Washington/Israeli efforts to isolate and punish Tehran for their own imperial gain.


Yet The Times said unnamed "Middle East experts" suspect "Iran and Hezbollah have denied involvement partly to distance themselves from the suspects who botched the plot, which had the appearance of sloppy amateurishness."


More likely, Mossad orchestrated them that way to assure Israelis weren't killed. When attacking Iranians, Palestinians, and other Muslims, targets nearly always die. Rarely do professional assassins miss.


Failing back to back in three countries raises obvious red flags. Israel perfected the art of killing. It's also skilled at manufacturing incidents avoiding them. Blaming Iran and Hezbollah for classic Israeli state terror is spurious. Yet screaming headlines highlight baseless accusations.


Notably Iran has close relations with India and Thailand. They're valued trading partners. New Delhi said Iranian oil purchases will continue. Moreover, a large trade delegation's coming to Tehran. Obviously the Islamic Republic has everything to lose and nothing to gain by launching terror attacks on Indian and Thai targets. It ludicrous to say so or against Georgia. Blame Mossad with everything to gain, not Iran.


London Guardian writer Arshin Adib-Moghaddam also called Iran "an unlikely culprit," saying:


If Iran wants to retaliate for Mossad's assassinating five nuclear scientists, "it has other means at its disposal. It is hard to imagine that (Tehran) would send Iranian operatives to friendly countries, completely equipped with Iranian money and passports - making the case against them as obvious as possible."


Israel and Washington both admit Iran's Revolutionary Guards are highly trained professionals. Why "would they launch such a clumsy and self-defeating operation?"


And why against three friendly countries at a time Washington/Israeli pressure targets the world community to isolate Iran.


Yet Israeli officials blamed Tehran. Netanyahu spuriously accused Iran of being "the biggest exporter or terror in the world." In fact, the Washington/Israeli/UK axis holds that distinction unchallenged.


Nonetheless, Netanyahu added that Israel "will continue, with local security, to act against the international terror which Iran produces." Foreign Minister Avigdor Lieberman made similar comments. So did other Israeli officials, pointing fingers away from themselves with major media support.


On February 19, Haaretz headlined, "US official: Signs pointing to increasing likelihood of Israel strike on Iran," saying:


As US National Security Adviser Tom Donilon arrived in Israel for talks on Iran's nuclear policy, "a senior US official" told Haaretz, "on condition of anonymity," that signs point to a likely Israeli strike. "We think that Israel still has not decided whether to attack or not," he said, "but it is clear to us that it is being considered seriously."


Washington wants more time to let sanctions bite harder. Netanyahu wants additional ones. According to a senior aide, "Any measure that doesn't stop Iran's nuclear program is inadequate."


In fact, claiming it's a red herring. Washington and Israel know it's non-military. America wants a pro-Western regime replacing Iran's independent one. Israel wants unchallenged regional dominance.


Both countries threaten war to achieve what world leaders should denounce. Instead, most go along subserviently, no matter the grave risks. As a result, humanity hangs in the balance.


Stephen Lendman lives in Chicago and can be reached at lendmanstephen@sbcglobal.net.

Tuesday, February 21, 2012

GRAND MAITRE LUAMBO LUANZO




RUANGWA YAKOSA FEDHA ZA MAENDELEO

Abdallah Bakari, Lindi

HALMASHAURI ya Wilaya ya Ruangwa mkoani Lindi, imekosa ruzuku ya fedha za maendeleo ya sekta ya kilimo kwa mwaka wa fedha wa serikali 2011/12, ilifahamika.

Akiwasilisha taarifa ya kilimo katika kikao cha kamati ya ushauri ya Mkoa wa Lindi, mshauri wa kilimo wa mkoa huo, John Likango alibainisha kuwa moja ya changamoto ya utekelezaji wa miradi ya kilimo katika mkoa huo ni pamoja na Wilaya ya Ruangwa kukosa fedha za kutekeleza miradi ya sekta ya kilimo (Dadps) kwa mwaka 2011/12.

Alisema hatua hiyo imefikiwa na Serikali kama adhabu, baada ya watendaji wilayani humo kushindwa kujibu hoja za Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Serikali juu ya matumizi ya Sh45 milioni katika idara ya kilimo.

Mwenyekiti wa halmashauri hiyo, Issa Libaba alikiri halmashauri yake kutotekeleza mradi wowote wa kilimo kwa mwaka huu, kutokana na kukosa fedha za ruzuku za maendeleo katika idara hiyo nyeti kulikosababishwa na watendaji wake kushindwa kujibu hoja za ukaguzi.

“Tulitarajia tupate Sh429 milioni kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika sekta ya kilimo wilayani kwangu, lakini kutokana na hoja hii hadi sasa hatujapata kiasi chochote cha fedha, tumeambiwa fedha hizo hatuwezi kupewa hadi hoja za ukaguzi zitakapojibiwa” alisema Libaba

Aliongeza kuwa “Sisi tunaendelea na utaratibu wa kuwachukulia hatua wale wote waliohusika, siku ukisikia mheshimiwa mwenyekiti (Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Ludovick Mwananzila) tunakuletea watendaji wako, wala usishangae, sisi hatuwezi kukaa nao tena”

Libabe huku akionekana mwenye kukerwa na tukio hilo alisema “Halmashauri yangu ilifukuzwa kwenye kikao cha Alat Taifa (kamati ya Bunge ya hesabu za Serikali za Mitaa), ni aibu tupu, wahusika watakapobainika basi hatutasita kuchukua hatua”




MWANANCHI.

MUBARAK'S WIFE THREATENS OBAMA OVER HER HUSBAND IMPRISONMENT

Suzanne Mubarak to Obama: Prevent the transfer of my husband to a prison hospital or I'll disclose the identities of U.S. agents.


Former Egyptian President Hosni Mubarak’s wife, Suzanne Mubarak, has sent U.S. President Barack Obama a threat that if he does not prevent the transfer of her husband to a prison hospital, she will disclose the identities of U.S. agents operating in Egypt.

The report on Suzanne Mubarak’s threat was posted on Monday to the website of the independent Israeli newspaper Megaphone. It quoted a report in the Egyptian newspaper Al-Mukhtasar.

According to the report, Suzanne Mubarak made it clear that she is very familiar with the identities and roles of American agents who operate in Egypt, due to her closeness to the Egyptian security elite. She reportedly threatened Obama that if he does not work against the current regime’s intention to transfer her husband she will reveal the information she knows.

Two weeks ago, Egyptian officials said that Mubarak will shortly be moved to the Tora prison in Cairo as soon as the facility is upgraded to house him.

Since his arrest last April, Mubarak has been held in custody first at a hospital in the Red Sea resort city of Sharm el-Sheikh and later at a military hospital outside Cairo.

Mubarak’s trial resumed in Cairo last month after having dragged on for months. The prosecutor later announced that he is seeking the death penalty for the man who led the nation for more than 30 years.

According to Egyptian media reports, Suzanne Mubarak fears that her husband's physical condition will deteriorate in the new prison, which may be the reason for her threats. Other reports said that Mubarak himself has hinted that if he is jailed in Tora, he will commit suicide.

Meanwhile on Monday, Egypt's General Prosecutor said that he had been unable to prove that any foreign power or organization had been involved in the violence against Egyptians during the uprising against Mubarak last year.

The prosecutor, Mustafa Suleiman, made the statement during closing arguments in the trial of Mubarak Monday.

One of Mubarak's lines of defense has been that the violence was incited by “foreign agents” who wanted to make him look bad, but Suleiman said that no evidence had been uncovered to implicate any outside intervention, not on the part of Israel, Iran, Hizbullah or Hamas. The responsibility for the violence rested solely on the shoulders of Mubarak and his administration.


ARUTZ SHEVA

Monday, February 20, 2012

WIZARA YA AFYA YAKANUSHA TAARIFA YA DCI KUHUSU MWAKYEMBE






WAZIRI ASEMA HAJAONA RIPOTI ALIYOWAPA WAANDISHI, AELEZA RIPOTI YA UGONJWA ANAYO DK MWAKYEMBE MWENYEWE, DK SLAA NAYE ASEMA ,"SINA IMANI NA MANUMBA"

WINGU zito limetanda kuhusu afya ya Naibu Waziri wa Ujenzi, Dk Harrison Mwakyembe baada ya Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Hadji Mponda, kusema kuwa ripoti ya ugonjwa wa Mwakyembe, anayo mwenyewe na kwamba wizara haina ripoti iliyotolewa na Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai, Robert Manumba, kwa waandishi wa habari.

Lakini wakati Dk Mponda akitoa kauli hiyo, baadhi ya watu wa kada tofauti wakiwamo viongozi wa dini na wasomi, wamekosoa ripoti hiyo ya polisi.

Mmoja wa watu hao, Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk Willibrod Slaa alisema,"hata mimi simwamini Manumba."

Malumbano hayo yanakuja wakati Dk Mwakyembe ambaye ni pia ni Mbunge wa Kyela, akitarajiwa nchini jana kwenda India kwa matibabu katika Hospitali ya Apollo.

Mahojiano na Waziri Mponda

Gazeti: Salaam Mheshimiwa waziri. Nimekupigia kutaka ufafanuzi kuhusu ripoti iliyotolewa na DCI Manumba kuhusu ugonjwa wa Dk Mwakyembe. Ninyi wizara mnaitambuaje?

Waziri: Kiutaratibu ripoti ya daktari ni ya mgonjwa. Sisi hatujaandika ripoti, muulizeni DCI Manumba awape ufafanuzi kama kuna kitu mnataka kuuliza zaidi kwa alichokizungumza na ninyi waandishi.

Gazeti: DCI Manumba alitoa taarifa kwa waandishi lakini aki-refer (rejea) ripoti kutoka wizarani (afya), baada ya kuwasiliana nanyi, kwa nini wewe usiizungumzie?

Waziri: Narudia tena, muulizeni yeye DCI au Dk Mwakyembe mwenyewe, wao wanaweza kuwapa ufafanuzi.

Gazeti: Tayari Dk Mwakyembe mwenyewe amekwishatoa tamko kwamba ripoti iliyosomwa na polisi, haina uhusiano na ripoti aliyokuwa nayo yeye kuhusu uchunguzi wa maradhi yake. Je, ripoti hii ya polisi ambayo wamedai wameipata kwenu (wizara) mmeitoa wapi?

Waziri: Ni hivi, baada ya daktari kumchunguza mgonjwa, hutoa ripoti na kumpa mgonjwa. Kwa hiyo, ripoti ya Hospitali ya Apollo anayo Dk Mwakyembe mwenyewe. Tena yeye kaeleza vizuri kabisa kwamba hata uchunguzi bado unaendelea. sasa hapo mnataka niseme nini tena?

Gazeti: Sasa kama ripoti anayo Dk Mwakyembe mwenyewe na tayari amesema ripoti ya polisi waliyosema imetoka kwenu siyo sahihi, je wizara iliwahi kupata ripoti ya Hospitali ya Apollo.

Waziri: Sisi tulichokifanya ni kumpa rufaa Dk Mwakyembe kwenda India. Ripoti hadi sasa anayo mwenyewe ingawa huwa tunapata taarifa baada ya yeye mgonjwa kuzileta kwetu. Hizo ndizo kanuni za taaluma ya udaktari, kwa hiyo ripoti anayo mwenyewe.

Gazeti: Sasa kama ripoti anayo Dk Mwakyembe mwenyewe, hii iliyosomwa na DCI imetoka wapi?

Waziri: Kumbuka DCI ana njia zake nyingi za kupata taarifa. Kwa hiyo ndiyo maana nasisitiza, muulizeni mwenyewe awape ufafanuzi kwa aliyozungumza na waandishi. Sisi wizara mnatuonea tu.

Gazeti: Lakini, hata kama ugonjwa ni siri, huoni mheshimiwa waziri kwamba kuna haja ya kuondoa utata kuhusu suala hili ikizingatiwa kuwa Dk Mwakyembe ni kiongozi anayegusa hisia za watu tofauti?

Waziri: Wanaoweza kuzungumzia maradhi yake, ni familia yake au yeye mwenyewe kwani ndiye mwenye ripoti. Mtafuteni au iulizeni familia yake iwapatie majibu. Lakini wizara haiwezi kufanya hivyo. Narudia tena, kuhusu hilo la DCI muulizeni mwenyewe awape ufafanuzi, mimi sijaona ripoti ya DCI aliyozungumza na waandishi wa habari.

Alichosema DCI

Akizungumza na waandishi mwishoni wa wiki iliyopita, Manumba alisema, “ukweli kuhusu kauli hiyo inayodai kuwekewa sumu, tumeupata baada ya kuwasiliana na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, ambayo nayo imewasiliana na hospitali aliyokuwa amelazwa Dk Mwakyembe nchini India. Taarifa zinaonyesha kuwa hakuna sumu."

Jana, alipoelezwa kwamba Dk Mwakyembe ameikana ripoti yao, Manumba alisema "sasa suala hilo litashughukiliwa kisheria."

Alisisitiza kuwa suala hilo litashughulikiwa kwa kufuata misingi ya kisheria na kwamba, Jeshi la Polisi haliko tayari kuendeleza malumbano kupitia vyombo vya habari.

"Hatua zaidi zinachukuliwa dhidi ya jambo hilo, kwa sasa litashughukiliwa kwa kufuata misingi ya kisheria kama nilivyokwishaeleza awali,"alisema Manumba.


Kauli ya Dk Mwakyembe

Juzi, akitoa tamko baada ya kukerwa na kauli ya Jeshi la Polisi alisema mbunge huyo alisema ‘napata taabu kuamini kama DCI Manumba na wenzake waliisoma taarifa halisi ya matibabu yangu au walisoma taarifa “nyingine”, na kama waliisoma taarifa hiyo wenyewe au “walisomewa”!

"Nasema hivyo kwa kuwa alichokisema DCI Manumba kwa waandishi wa habari, hakifanani kabisa na picha iliyoko kwenye taarifa halisi ya Hospitali ya Apollo inayotamka wazi kuwa kuna kitu kwenye bone marrow kinachochochea hali niliyonayo, kitu ambacho mabingwa wanahangaikia kukijua, kukidhibiti au kukiondoa huku vyombo vyetu vya dola vikipelekeshwa na mafisadi kusema bila msingi wa kisayansi wala aibu: “hakulishwa sumu”, “hakulishwa sumu”

Dk Mwakyembe pia alitoa sababu kuu tatu za kupinga ripoti o ya DCI akisema:

"Kwanza, kwa kuingilia mchakato wa matibabu yangu na uchunguzi wa kina kuhusu kiini chake, unaoendelea katika Hospitali ya Apollo, nchini India, ambako bado sijahitimisha matibabu yangu, pili kwa ufinyu wa uelewa unaojitokeza bayana kwenye tamko la Jeshi la Polisi unaosisitiza kuwa “sikunyweshwa sumu” wakati sumu si lazima unyweshwe ili ikudhuru, inaweza kudhuru hata kwa kugusishwa tu.

Alisema sababu ya tatu ni kitendo cha Jeshi la Polisi kujiingiza kwenye suala ambalo kwa takriban mwaka mzima sasa, halijawahi kuwa na dhamira ya dhati ya kulielewa au kulichunguza mbali na kulifanyia mzaha kupitia magazetini.

Dk Slaa

Akizungumzia sakata hilo, Dk Slaa alisema hana imani na ripoti ya uchunguzi iliyofanywa na Jeshi la Polisi na kutolewa na Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai, kuhusu hali ya Mwakyembe.

"Mimi siwezi kuzungumzia ugonjwa wa mtu, lakini niseme tu kwa kifupi kuwa ripoti ya DCI Manumba siwezi kuiamini. Sina imani na Manumba kwa sababu mimi mwenyewe imenitokea,"alirusha kombora kwa Manumba.


"Niliwekewa vipaza sauti kwenye kitanda changu mjini Dodoma, taarifa za tukio hilo zilifika kwake lakini hadi leo hajatoa majibu yoyote ya uchunguzi wake," alisisitiza.

"Nani asiyemfahamu Manumba ndiye alishuhudia watu 50 wakipoteza maisha kwa kufukiwa mgodini na kesi ikaenda mahakamani, ikafutwa, Kwa nini Serikali yetu inamweka mtu wa aina hiyo kwenye nafasi kubwa kama hiyo," alihoji Dk Slaa.

Alisema hata katika tukio la kuwekewa vinasa sauti kwenye kitanda huko Dodoma, hakuwahi kuitwa na kuhojiwa.

Askofu Ruwa'ich
Akizungumzia mvutano huo, Rais wa Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC), Yuda Thadeus Ruwa'ichi, alisema kinachoendelea kati ya jeshi na Dk Mwakyembe, ni ishara ya kutosha kuwa taifa liko kwenye ubabaishaji.

"Malumbano hayo yanaonyesha kuwa taifa liko kwenye ubabaishaji na hiki siyo kitu kizuri. Ushauri wangu turudi na kuwa wakweli, tufanye kazi kwa uadilifu,"alisema askofu Ruwa'ichi.

Rais huyo wa TEC, pia aliwataka waandishi wa habari kufanya uchunguzi wao na kutoa taarifa za kubaini ukweli kuhusu jambo hilo, ili kuondoa utata uliopo.

Jukwaa la katiba

Mwenyekiti wa Jukwaa la Katiba, Deus Kibamba alielezea kushangazwa kwake juu ya nguvu aliyopata Manumba ya kupishana na mawaziri.
Alisema kinachotakiwa ni jopo la madaktari bingwa wa nchini, kuunda tume ili kuja na jibu litakalowawezesha wananchi waache kuihofia Serikali.

"Mabishano baina ya viongozi wa Kikwete (Rais), yanaonyesha dhahiri kwamba Serikali ina ulegevu, unaotokana na kiongozi wake mkuu kukaa kimya," alisema.
Kibamba alisema wakati umefika kwa Rais wa nchi kujitokeza hadharani na kuwawajibisha mawaziri, kama anaamini kuwa yanayoongelewa ni ya uwongo.
“Kilichoelezwa na Manumba hakiingii akilini kwa mwananchi wa kawaida, hii nchi sasa ni ya kisanii maana umegeuka mchezo wa Bongo land wa kuongea bila kuthitibishwa na madaktari bingwa,”alisema.

“Afya za mawaziri si suala la siri hasa ikizingatiwa kuwa wanatumia fedha za Watanzania katika kutibiwa . Kama kiongozi anataka kuweka siri aondoke kwenye uongozi atumie fedha zake,” alisisitiza.

“Siamini kama DCI Manumba ni daktari , kinachotakiwa ni kuundwa jopo la madaktari bingwa na Rais kuwaeleza Watanzania kinachowasibu viongozi wake,” aliongeza.

Alisema Watanzania wanaamini kuwa Dk Mwakyembe alilishwa sumu na kwamba ni vema Serikali ikaondoa mkanganyiko huo.


Akizumngumzia sakata hilo kwa njia ya simu, Mbunge wa Nyamagana, jijini Mwanza, Hezekiah Wenje alisema ni dhahiri kwamba kuna kitu ambacho Jeshi la Polisi linakificha.

“Hali halisi inaonyesha wazi kuwa kuna ukweli mwingi unaofichwa na Jeshi la Polisi na ndiyo maana kunakuwa na upotoshaji wa wazi,” alisema Wenje.

Mbunge huyo alisema kuna haja sasa ripoti ya madaktari kuwekwa wazi ili watu wajue.

Kwa upande wake, wakili wa kujitegemea mkoani Mwanza, Stephen Magoiga alisema Jeshi la Polisi, linaonyesha wazi kwamba lina matatizo makubwa ya kiutendaji linapotaka mlalamikaji kuwasilisha ushahidi.

Akikumbushia Dk Mwakyembe kudaiwa ushahidi alipopeleka malalamiko yake juu ya maisha yake kuwa hatarini, Magoiga alisema ushahidi ni suala la kitaalamu ambalo si mtu yoyote anaweza kukusanya.

“Jeshi la Polisi ndilo lenye utaalamu wa kukusanya ushahidi na wanalipwa kwa kazi hiyo, sasa wanapodai mlalamikaji alete ushahidi na baadaye kupingana na madai yake, ni dhahiri kwamba jeshi hilo linasema uwongo,” alisema Magoiga.

Alisema polisi wanapaswa kufanya kazi kisayansi kwa kuzingatia kwamba tuhuma za Dk Mwakyembe kulishwa sumu zimetolewa mara ya kwanza na mtu mzima mwenye hadhi yake katika jamii ya Kitanzania.

Alisema ni jambo la kushangaza kuona polisi wakioonyesha dharau za waziwazi kwa tuhuma zilizotolewa na mtu kama Waziri Samwel Sitta.

“Kama kauli ya Sitta inaweza kutendewa hivi na polisi je, ya mtu wa kawaida itakuwaje," aliohoji wakili huyo.


Ijumaa iliyopita Manumba alitoa tamko kuhusu kauli zilizowahi kutolewa na Sitta akiziita kuwa ni za uwongo na kuwataka watu wazipuuze.

Pia alitishia kuchukua hatua za kisheria dhidi ya Waziri huyo wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Gaudence Mpangala, alisema mabishano yanayoendelea ndani ya Serikali, yanaonyesha kuwa kuna kitu kinachofichwa.
Profesa Mpangala alihoji kuhusu mahali ambako kumpa nguvu Manumba kuongelea afya ya Dk Mwakyembe.

Alisema kitendo hicho kinapingana na msimamo wa Waziri Mkuu Mizengo Pinda ambaye aliwahi kukaririwa akisema Dk Mwakyembe ndiye anayepaswa kueleza hadharani maradhi yanayomsumbua.

Alisema Jeshi la Polisi limedharau kauli ya Pinda na kwamba hiyo inaonyesha kuwa Serikali, imekosa msemaji wa mwisho.

Sheikh wa Mkoa wa Dar es salaam
Shehe Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Alhad Musa Salim, alisema hatua ya viongozi kupishana inaonyesha kuwa hawafanyi kazi kwa umoja.

“Kilichoongelewa na Jeshi la Polisi ni sahihi kwa sababu limepewa jukumu la kuchunguza na kama kuna viongozi hao wanapinga majibu hayo, nadhani wanapaswa kuja na jibu,” alisema.

“Mimi sijui chochote lakini kama unachoeleza ni hivyo, maoni yangu ni kwamna tunatakiwa kuheshimu uchunguzi wa polisi ambao wamepewa dhamana ya kuchunguza,” alisema Sheikh Salim.


Historia ya ugonjwawa Mwakyembe
Dk Mwakymbe alianza kuumwa Oktoba 9 mwaka jana na baadaye kupelekwa India ambako alilazwa katika Hospitali ya Apollo kwa matatibu.

Alirejea nchini Desemba 11 mwaka jana, baada ya kulazwa hospitalini kwa takribani miezi miwili.


Msemaji wa familia ya Dk Mwekyembe ambaye ni Mbunge wa Lupa, Victor Mwambalaswa alisema mara baada ya mbunge huyo wa Kyela kuwasili nchini kuwa, afya yake ni nzuri na ndio maana ameruhusiwa kutoka hospitalini.

Kauli za Waziri Sitta

Mara kadhaa Waziri Sitta amekuwa akinukuliwa na vyombo vya habari akisisitiza kuwa ugonjwa wa Dk Mwakyembe, umetokana na kulishwa sumu.

Akiwa kwenye uzinduzi wa Programu ya Neno la Hekima kutoka kwa kiongozi, iliyoanzishwa na Kanisa la Ufufuo na Uzima la Kawe, Jijini Dar es Salaam Januari 28 mwaka huu, Sitta alisema “ Dk Mwakyembe kapewa sumu, kama vyombo vya uchunguzi vinasema siyo, basi watueleze ukweli, tena haraka.”

“Ni vipi uone binadamu ambaye ukimshika katika ngozi unga unamwagika chini, mhudumu anakuja kuufagia, lakini baada ya saa moja unarudia tena, kitu hicho si cha kawaida,” alisisitiza Sitta.

Sitta alisema wamejaribu wameshindwa kwa kuwa Dk Mwakyembe analindwa kwa jina la Yesu ambalo ni kubwa kuliko yote.

Waziri Nahodha

Hata hivyo, akijibu moja ya kauli hizo, Waziri wa Mambo ya Ndani, Shamsi Vuai Nohodha alimtaka Waziri Sitta awasilishe ushahidi wake ili ufanyiwe kazi badala ya kuzungumza nje ya vyombo vya sheria.

Lakini, Sitta alisema hatapeleka ushahidi kuhusu madai kwamba Dk Mwakyembe alilishwa sumu kwa kuwa polisi tayari wana ushahidi.

Alilaumu kuwa hata yeye aliwahi kupeleka tuhuma za kutaka kuawa lakini alipuuzwa.



Alisema inachotakiwa kufanywa na polisi ni uchunguzi kuhusu madai ya Dk Mwakyembe kulishwa sumu.

“Waziri Nahodha anataka ushahidi gani ikiwa taarifa za madaktari zinazomhusu Dk Mwakyembe kuhusu sumu aliyopewa zilishapelekwa polisi, anataka mimi nitoe ushahidi gani,” alisema Waziri Sitta.

Habari Ray Naluyaga, Mwanza Geofrey Nyang'oro na Keneth Goliam
a



MWANANCHI



TAARIFA YA DK. MWAKYEMBE KWA VYOMBO VYA HABARI



Dk. Harrison G. Mwakyembe (Mb), NW-UJ

Dar es Salaam

18/02/12

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Nimelazimika leo Jumamosi, tarehe 18 Februari, 2012 kutoa taarifa hii kwa vyombo vya habari kufuatia mkutano wa DCI Robert Manumba na waandishi wa habari jana (17/02/12) kuongelea, pamoja na mambo mengine, hali yangu ya afya na kuhitimisha, kienyejienyeji tu kuwa “sikunyweshwa sumu” ila naumwa tu ugonjwa wa ngozi bila kufafanua ugonjwa huo wa ngozi umesababishwa na nini!

Napenda nisisitize mapema kabisa kuwa msimamo huo wa Jeshi la Polisi umenikera sana katika hali niliyonayo ya ugonjwa, kwanza kwa kuingilia mchakato wa matibabu yangu na uchunguzi wa kina kuhusu kiini chake unaoendelea hospitali ya Apollo nchini India ambako bado sijahitimisha matibabu yangu; pili kwa ufinyu wa uelewa unaojitokeza bayana kwenye tamko la Jeshi la Polisi unaosisitiza kuwa “sikunyweshwa sumu” wakati sumu si lazima unyweshwe ili ikudhuru, inaweza kudhuru hata kwa kugusishwa tu; na tatu kwa Jeshi la Polisi kujiingiza kwenye suala ambalo kwa takriban mwaka mzima halijawahi kuwa na dhamira ya dhati ya kulielewa au kulichunguza mbali na kulifanyia mzaha kupitia magazetini.

Itakumbukwa kuwa tarehe 9 Februari, 2011 nilimwandikia barua IGP Said Mwema kumtaarifu kuhusu njama za kuondoa maisha yangu na ya viongozi wengine. Kwa kutambua kuwa Jeshi la Polisi la Tanzania daima husisitiza kuletewa ushahidi kwanza ndipo lifanyekazi, nilihakikisha nimeainisha katika barua hiyo kila ushahidi nilioupata au kupewa. (Utaratibu huu wa Jeshi la Polisi kusubiri kuletewa ushahidi mezani, kama ambavyo mahakimu wanavyosubiri ushahidi mahakamani, haupo popote pale duniani (ila Tanzania tu) kwani kazi ya msingi ya Polisi si kuletewa, ni kutafuta ushahidi. Polisi wanachohitaji duniani kote ni kupata clue au tetesi tu. Hiyo inatosha kufukua ushahidi wote unaohitajika). Pamoja na kujitahidi kuanika kila aina ya ushahidi niliokuwa nao, mambo manne yalijitokeza ambayo yalionyesha wazi kuwa Polisi hawakuwa na dhamira ya dhati ya kupeleleza suala hilo:

(i) Siku chache baada ya kumkabidhi IGP barua hiyo, nilitumiwa timu ya “wapelelezi” ofisini kwangu kuja kuchukua maelezo yangu ya ziada. Timu hiyo ilikuwa inaongozwa na ACP Mkumbo, afisa wa polisi ambaye wiki chache zilizokuwa zimepita alikuwa miongoni mwa askari waliotuhumiwa kupokea rushwa kwa lengo la kumbambikizia madawa ya kulevya mtoto wa Mwenyekiti wa IPP, Reginald Mengi, suala ambalo mpaka leo hii uongozi wa Polisi umeshindwa kulitolea maelezo ya kuridhisha. Kwa msingi huo, nilikuwa nimeletewa mtuhumiwa wa rushwa/ ujambazi kuendesha uchunguzi wa watuhumiwa wengine wa ujambazi! Nikatambua mara moja kuwa zoezi zima lilikuwa la mzaha, tena mzaha mkubwa!

(ii) Wiki chache baada ya barua yangu kuwasilishwa kwa IGP na timu ya ACP Mkumbo “kuanza kazi”, Jeshi la Polisi likachukua hatua ya kuwapongeza na kuwazawadia askari niliowatuhumu kushirikiana na majambazi! Huhitaji kuwa profesa wa falsafa kuelewa kuwa huo ulikuwa ujumbe tosha wa kunipuuza.

(iii) Hivi karibuni tuhuma za askari polisi kujihusisha na vitendo vya ujambazi mkoani Morogoro zilipopamba moto na kuwagusa askari “wale wale” niliowatuhumu kwenye barua yangu, IGP alichukua hatua ya kuwahamishia mikoa mingine!

(iv) ili kunikatisha tamaa kabisa, barua yangu ya “siri” kwa IGP ikavujishwa kwa makusudi kwenye vyombo vya habari na kuchapishwa kama habari ambayo ilikebehi na kukanusha taarifa nzima niliyotoa, sijui kwa faida ya nani! Lakini huu ni mchezo wa kawaida kwa polisi kwani hivi karibuni Mhe. Waziri Samuel Sitta alipohojiwa na ofisa mwandamizi wa Jeshi la Polisi ofisini kwake, wakiwa wawili tu, taarifa ya kikao hicho ikawa kwenye moja ya magazeti ya mafisadi ikikebehi ushahidi aliotoa Sitta! The integrity of the police force leadership is on the line.

Nimeelezea vizuri katika barua yangu kwa IGP kuwa kundi hilo la mauaji lilikuwa limeelekezwa kuniua kwa kutumia sumu, taarifa ambayo kwa karibu mwaka mzima Polisi hawakutaka kuifuatilia kwa sababu wanazozijua wenyewe. Sasa huu msukumo mpya wa Jeshi la Polisi kutaka kujua kama nilipewa sumu au la na kukurupuka kutoa tamko hata kabla ya kunichunguza nilivyo, kunihoji mimi na wasaidizi wangu ofisini na hata kuongea na mabingwa wa Kihindi wanaonifanyia uchunguzi, umetokea wapi? Si ni polisi hawahawa ambao, badala ya kushukuru, wamekuwa wakikerwa na tahadhari ambazo Waziri Sitta amekuwa akitoa ili suala hili lichunguzwe kwa kina?

Aidha napata taabu kuamini kama DCI Manumba na wenzake waliisoma taarifa halisi ya matatibabu yangu au walisoma taarifa “nyingine”, na kama waliisoma taarifa hiyo wenyewe au “walisomewa”! Nasema hivyo kwa kuwa alichokisema DCI Manumba kwa wandishi wa habari hakifanani kabisa na picha iliyo kwenye taarifa halisi ya Apollo ambayo inatamka wazi kuwa kuna kitu kwenye bone marrow kinachochochea hali niliyonayo, kitu ambacho mabingwa wanahangaikia kukijua, kukidhibiti /kukiondoa huku vyombo vyetu vya dola vikipelekeshwa na mafisadi kusema bila msingi wa kisayansi wala aibu: “hakulishwa sumu”, “hakulishwa sumu”!

Nimesoma darasa moja Kitivo cha Sheria Mlimani na DCI Manumba. Baadaye IGP Mwema alikuwa mwanafunzi wangu wa sheria Mlimani. Vigogo hawa wawili wa usalama wa raia nchini hawajanitendea haki, nao wanajua. Wanajua vilevile kuwa sitakaa kimya au kumung’unya maneno come what may pale ambapo haki inakanyagwa.

Tuendelee kuombeana afya na uhai ili tutendeane haki na vilevile tuitendee nchi yetu haki kwa kuvimalizia viporo vinavyokera vya Dowans, EPA, Kagoda n.k. kwa maslahi mapana ya Taifa letu.

Mungu Ibariki Tanzania.

Saturday, February 18, 2012

KUFELI HUKU NI JANGA LA TAIFA SI SUALA LA WAKRISTU VS WAISLAMU



WAKATI mwingine natamani ningekuwa na uwezo wa kuwatia bakora baadhi ya watu wanaozungumzia suala la maelfu ya wanafunzi kufeli vibaya katika mtihani wa kidato cha nne.

Watu wanaoniudhi na kunikera ni wale ambao wanayaangalia matokeo haya ya mtihani kama ni suala la ubora wa shule za “Kikristu” kulinganisha na shule za “Kiislamu” au wale wanaoona “kupendelewa kwa Wakristu” na “mfumo Kristu”.

Mwitikio wa baadhi ya watu kufuatia kutangazwa kwa matokeo ya kidato cha nne kwa kweli unanifanya nijiulize kama udini umezama kati yetu kiasi kwamba hatuoni kilichotokea na kinachotokea katika elimu ni nini.

Ndugu zangu, kuna janga katika sekta ya elimu ambalo linasababisha maelfu ya watoto wetu, wadogo zetu, ndugu zetu kuachwa nje ya elimu! Jamani, hawa maelfu wanaofanya vibaya si Waislamu, si Wakristu, si Wapagani hawa ni Watanzania!

Kwa upande wa Wakristu

Kuna baadhi ya Wakristu ambao wanapoangalia matokeo ya mitihani wanajisikia vizuri kwamba watoto wenye majina ya Kikristu wanaonekana kuwa wamefanya vizuri.

Tena wengine wanajisikia vizuri wanapoona majina ya shule zilizofanya vizuri mengi yanahusiana na Wakristu na hivyo kuthibitisha ile imani kwamba shule za Kikristu ni bora. Sasa, jambo moja liko wazi sana kwamba shule za Kikatoliki – si shule za majina ya Kikristu tu -karibu sehemu zote duniani zinatoa elimu ya kipekee na bora zaidi.

Hilo ni kweli India, China, Pakistani, Uingereza, Marekani na hata Indonesia. Kuna sababu ya hilo na si kusudio langu kuingia kwa undani kwenye sababu hizo. Sasa huu ni ubora unaotokana na mfumo wa elimu ya Kikatoliki pote duniani na hili halikuanza jana au juzi. Kanisa Katoliki lina historia ya muda mrefu katika masuala ya elimu mbalimbali huko Ulaya na baadaye katika makoloni ambayo yalichukuliwa na nchi za Ulaya.

Nimesema hili ili kusiwe na hisia kuwa ni shule za Kikatoliki za Tanzania ndizo zinafanya vizuri zaidi. Wale wanaowaaminisha watu kuwa shule za Kikatoliki za Tanzania zinafanya vizuri zaidi kwa sababu “zinapendelewa” hawawatendei haki wasikilizaji wao.

Mtu anaweza kwenda Kenya, Zambia, Uganda, Nigeria au nchi yoyote ambayo ina mfumo wa shule za Kikatoliki na ataona kuwa shule hizi zinafanya vizuri zaidi na mara nyingi kuliko shule nyingine binafsi au za serikali.

Lakini si watoto wote wa Kikristu wanasoma shule za Kikristu! Si Wakatoliki wote hupeleka watoto wao kwenye shule za Wakatoliki kwanza kwa sababu zina gharama ya juu na vile vile kwa sababu ni chache na zina uchaguzi wa hali ya juu sana.

Hii ina maana ya kwamba bado kuna Wakristu (Wakatoliki na wengine) ambao wanapeleka watoto wao kwenye shule hizi hizi za umma. Maelfu ya hao waliofeli kwa mara nyingine ni Wakristu vile vile na hivyo huku si kufeli kwa watoto wa Kiislamu peke yake kama watu wengine wanavyochukulia.

Kwa Waislamu

Wale Waislamu ambao wanaangalia suala hili kama ni mashindano ya “sisi dhidi ya nyinyi” hawawatendei haki watoto wa Kiislamu nchini. Kuwaambia au kuwafanya watoto waamini kuwa wamefeli kwa sababu ni Waislamu ni kuwaonea, kwani hao watoto wanajua – kama wanatazama vizuri – kwenye shule hiyo hiyo waliyofeli wao watoto wengine mamia wa Kikristu nao walifeli!

Hawa Waislamu wanaofikiria kuwa Wakristu wote nchini wanapata elimu nzuri, wanapata kazi nzuri na wanaishi maisha yenye utu na kuwa Waislamu wote hawajasoma na hawana nafasi yoyote ya maana na kuwa hakuna Waislamu wengine wanaofanya vizuri kwenye mitihani, hawautendei haki ukweli.

Sote tunajua wapo Waislamu ambao wamefanikia na wanaendelea kufanikiwa kwa kila kipimo; wapo wafanyabiashara, wasomi, walimu, madaktari n.k ambao ni Waislamu ambao wamesoma kwenye elimu hii ambayo Wakristu wengine wanapata. Sasa kufeli kwa baadhi ya shule za Kiislamu ni lazima kutafutiwe maelezo ya kisayansi kama vile kufeli kwa shule za Kata au shule nyingine binafsi kunavyohitaji maelezo.

Nitoe mifano kidogo

St. Mary ya Mbalizi huko Mbeya ni shule inayoonekana ina jina la Kikristu na sijui kama ni ya kanisa au mtu binafsi. Mtu mwingine anaweza kufikiria labda shule hiyo imefanya vizuri. Matokeo ya mtihani shule hiyo yanaonyesha kuwa waliopata daraja la 1 ni 0 waliopata daraja la 2 ni 0 waliopata daraja la tatu ni 1 na waliopata daraja la nne ni 38 huku 34 wakifeli. Huo mfumo Kristu umeshindwa vipi kuwasaidia hawa?

Shule nyingine inaitwa St. Margareti ya wasichana. Sasa kwa jina na kwa vile ni ya wasichana tena wengi wana majina ya Kikristu watetezi wa hoja ya “mfumo Kristu” wangeweza kutuonyesha kuwa shule hiyo wanafunzi wake wameshinda kwa kiwango cha seminari za kiume. Hakukuwa na mtoto yeyote aliyepata daraja la kwanza, la pili wala la tatu! Walikuwepo 27 wa daraja la nne na 28 wakifeli kabisa!

Shule nyingine ni St. Paul ambayo nayo kwa kuangalia haraka haraka tunaweza kuamini kuwa ni shule ya Kikristu na hivyo ingependelewa na mfumo “Kristu”. Wanafunzi wengi wana majina ya Kikristu lakini katika shule hiyo hakuna hata mmoja aliyepata daraja la kwanza, la pili au la tatu!

Sasa hii ni mifano michache tena ya haraka haraka tu kuonyesha kuwa wanaofeli si watoto wa Kiislamu tu na si katika shule zenye majina ya Kiislamu tu! Wanaojaribu kuelezea kufeli huku kwa misingi ya kidini hutawasikia wakiwapigania watoto hawa wa Kitanzania! Wao wameng’ang’ania “mfumo Kristu, mfumo Kristu” na hawa watoto walilie nini? Rais Muislamu? Makamu Muislamu? Ndipo maelezo ya kufeli kwao yatapatikana?

Tuvuke mpaka wa udini na kuliangalia tatizo letu kama letu sote

Ndugu zangu, muda wa kubebesha lawama za kidini tena za kijinga umepita. Watoto wetu wanafeli kila mwaka na sisi watu wazima tumekaa kama washirikina kukwepa kuelezea mambo yanayoelezeka kisayansi na badala yake tunatafuta maelezo mepesi yasiyoweza hata kushawishi akili za mtoto mdogo.

Wazazi wa Tanzania ni lazima wakasirike kuwa watoto wao wengi wanafeli na wanapoteza nafasi. Hivi tumewahi kujiuliza hawa watoto wote wanaofeli kila mwaka na wakakosa nafasi ya kuendelea mbele huwa wanaenda wapi? Hivi, tunafikiria wote wanaenda kwenye shughuli gani hasa? Hawa watoto wa kike ambao walijizuia na majaribu mbalimbali ili angalau wapate elimu ya sekondari wanapofeli nani anajali!?

Binafsi naomba niwe wa kwanza kutaka uongozi wote wa Baraza la Mitihani kujiuzulu na pamoja nao kufumuliwa kwa uongozi wa Wizara ya Elimu. Hizi sera za CCM zimekuwa janga la kudumu sasa na watu wetu hawachoki na hawakomi! Leo hii vile ambavyo vimekuwa aibu na fedheha kwa familia nyingi vimekuwa navyo ni aibu hadi Ikulu! Nani atatusadia?

Makundi ya Waislamu wanadai Wakristu wanapendelewa; Wakristu wanasema Waislamu hawapendi elimu. Lakini ukweli unabakia kuwa wanaofeli na kupoteza nafasi nyingi ni watoto wa Kitanzania, Waislamu, Wakristu, Wapagani na wasioamini kabisa!

Tufanye nini? Well, wapo wanaoangalia CCM na serikali yake kutafuta majibu. Hatuamini kuwa tunavuna tulichopanda; hatutaki kukubali kuwa haya ni matokeo ya kushindwa kwa sera za elimu pamoja na mipango yake yote!

Tunatumia mabilioni ya shilingi kila mwaka lakini tunazidi kufelisha kama tuna wazimu au tunashindana. Hadi inafika wakati watoto wanaandika mashairi ya bongo flava kwenye mitihani na watu bado wako na ofisi zao wakisubiri mwaka mwingine, hakuna hasira, hakuna kukerwa, hakuna kuchukizwa, inashangaza!

Hivi walimu na wenyewe kwa nini wasigome hadi mabadiliko ya kweli yaanze? Walimu wanaweza na wanapata wapi ujasiri wa kwenda darasani na kukuta shule isiyo na milango, madawati, vitabu na watoto ambao wamekosa chakula? Mwalimu anaweza kufundisha vipi mahali ambapo mtoto akirudi nyumbani hana cha kufanya zaidi ya kujipanga kucheza “Hakunaga”?

Hawa wazazi wanaoshabikia mtoto “anavyojua kucheza sana” wanafikiria watoto watafaulu kwa kuombea au kwa kuonea? Wazazi wangapi wanauliza kama mtoto kamaliza kazi na kufuatilia kuona amefanya kazi yake vizuri? Wazazi wenyewe ni nani anawasaidia kuweza kuwasaidia watoto maana si wazazi wote nao wana uwezo wa kusaidia watoto wao linapokuja suala la shule. Kama mzazi hakupata elimu yeye mwenyewe anaweza vipi kufuatilia elimu ya mtoto wake?

Labda sasa inabidi tufikirie kitu kingine nje ya CCM, nje ya sera hizi zilizoshindwa na nje ya watu hawa hawa. Tufanye nini? Tusaidie vipi? Au tukubali tu na kuombea labda mwaka ujao tutafaulisha zaidi kidogo. Twende tukaombee na kwenda kwa waganga tuone ni nani anatuloga! Maana kama hatutaki kutumia vichwa vyetu na uwezo wetu tuliojaliwa na Mwenyezi Mungu kubadilisha maisha yetu hivyo ni bora tuanze kutumia uganga wa kienyeji!?

Vinginevyo, kuna kitu cha haraka, cha makusudi na kikali kinahitajika kufanyika ili kuokoa elimu ya watoto wetu. Lakini ili tuweze kufika ni lazima kwanza tukasirike. Mimi nimekasirika na nimekerwa. Sijui wewe mwenzangu unajisikiaje? Kama hujisikii hasira yoyote au kukerwa kwa namna yoyote, nina uhakika wewe ni sehemu ya tatizo!


RAIA MWEMA

Friday, February 17, 2012

MBOWE: DR SLAA RUKSA KUGOMBEA ARUMERU





ALIYEPEPERUSHA BENDERA CHADEMA 2010 AREJEA KUTOKA MAREKANI, AUNGA MKONO


Musa Juma na Moses Mashalla, Arusha
WAKATI Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa akianza kugusa hisia za watu wanaomtaka agombee ubunge katika Jimbo la Arumeru Mashariki, mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe amesema iwapo mtendaji mkuu huyo wa chama ataamua kuwania kiti hicho, wataheshimu uamuzi wake.

Wakati Mbowe akitoa kauli hiyo, aliyepeperusha bendera ya Chadema katika uchaguzi wa mwaka 2010, Joshua Nasari na kutoa upinzani mkali kwa mgombea wa CCM, marehemu Jeremiah Sumari, naye amesema kama katibu mkuu wake ataamua kuwania kiti hicho, hatakuwa na pingamizi ikiwa chama kitaamua kwani lengo ni kutwaa jimbo hilo.

Akizungumza na Mwananchi jana baada ya kuibuka mjadala kuhusu uwezekano wa Dk Slaa kuwania jimbo hilo, Mbowe alisema, "Katika suala la kugombea, utashi binafsi ni jambo la msingi...,kama Dk Slaa ataamua kugombea ubunge Arumeru Mashariki, tutaheshimu uamuzi wake."

Mbowe alisema katika uteuzi wa chama, kuna vigezo vinavyoangaliwa ikiwa ni pamoja na jinsi mtu anavyokubalika kwa wananchi anakogombea, sifa zake na utashi wake binafsi na kuongeza, "Hatuna uteule katika chama."

Hata hivyo, Mbowe alisema Chadema hakiwezi kumlazimisha Dk Slaa akagombee jimbo hilo kama mwenyewe utashi haumtumi kufanya hivyo, na kwamba hana shaka na kukubalika kwa katibu mkuu huyo kutokana na imani aliyojijengea kwa umma wa Watanzania.

Mbowe alisema Dk Slaa amekuwa akiombwa kugombea ubunge katika maeneo mengi likiwamo Jimbo la Igunga, lakini chama kisingeweza kumlazimisha kwani jambo la kwanza ilibidi mwenyewe aonyeshe utashi binafsi wa kutaka kuwania kiti hicho.

"Dk Slaa aliwahi kuombwa akagombee Igunga, lakini hakwenda. Hii ni kwasababu anakubalika nchini karibu kote, hivyo kama atakuwa na utashi binafsi kwanza, nadhani taratibu za chama zitatumika tu kufikia uamuzi," alifafanua.

Mwenyekiti huyo wa Chadema pia alitoa angalizo kwamba, wakati mwingine uamuzi wa chama kupata mgombea unaangalia jinsi mgombea alivyo na mtandao katika jimbo analotaka kugombea ili hata kama akichaguliwa aonekane ni mbunge wa eneo hilo.

"Ndiyo maana nasema kuna vigezo vingi tu, kwa mfano mtu anaweza kuwa mbunge mzuri bungeni, lakini je, ana connectivity (kinachomuunganisha) jimboni, kuangalia kama ana makazi na mtandao mwingine kwani asije akawa mbunge mzuri bungeni, lakini jimboni akiwa kama mgeni hivyo watu wakaona kama kimewapelekea pandikizi tu,"alifafanua Mbowe.

Tangu juzi kumekuwa na mjadala katika mitandao ya kijamii huku baadhi wakimtaka Dk Slaa akagombee ubunge Arumeru Mashariki kuziba pengo la aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Marehebu Sumari, lakini wengine wanapinga na kumtaka aendelee kubaki na nafasi yake ya katibu mkuu wa chama kwa lengo la kukijenga.

Hata hivyo, Dk Slaa ambaye katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010 alishika nafasi ya pili akiwa nyuma ya Rais ya Jakaya Kikwete, juzi alinukuliwa na gazeti moja la kila siku (siyo Mwananchi) akisema, "Siwezi kulizungumzia jambo hilo, maana nilikwisha kusema muda mrefu kuwa sitaki tena ubunge na isitoshe mimi si mwenyeji wa Arumeru,"

Joshua Nasari
Kwa upande wake Nasari (26) ambaye ana mtaji mkubwa wa kura kufuatia matokeo ya uchaguzi wa mwaka 2010 alitoa msimamo wake akisema yupo tayari kufanya mazungumzo na viongozi wa juu ya chama chake juu ya kumpisha Dk Slaa kuwania ubunge katika jimbo hilo kama akihitaji.

Nasari ambaye amerejea hivi karibuni mjini Arusha akitokea nchini Marekani, leo anatarajiwa kuchukua fomu rasmi ili kuwania nafasi hiyo kupitia Chadema.

"Nimesikia maoni kupitia mitandao na wadau wakimuomba Dk Slaa kugombea, hili ni jambo jema kwetu kwani wananchi wanajua jimbo hili tunashinda Chadema na kama Dk (Slaa) akitaka kugombea dekomrasia ya chama chetu itafanya kazi, kwani kikubwa tunataka ushindi,"alisema Nasari.

Nasari aliyewahi kuwa Waziri Mkuu katika Serikali ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Daruso) kati ya 2008 na 2009 alipohitimu shahada ya Sayansi ya Jamii katika masuala ya utengenezaji Sera na Utawala, alisema ana imani Chadema kitashinda Arumeru.

"Nilikuwa Marekani kikazi na sasa nimerejea kama ulivyoshuhudia watu wengi wananiunga mkono na tayari wamenichangia Sh 11milioni za kampeni na magari manane," alisema Nasari.

Mgombea huyo ambaye tayari ametangaza kuacha kazi katika shirika la Kimarekani la Foundation For Tomorrow ili kujikita kwenye uchaguzi huo, alisema wakazi wa Arumeru Mashariki wanahitaji mwakilishi sahihi ambaye anaweza kuwatetea katika kuinua uchumi wao.

Hata hivyo, alisema tayari amepata taarifa za Dk Slaa kutoa tamko kuwa hawezi kushiriki katika uchaguzi huo, kwa kuzingatia kuwa sio mkazi wa Meru na pia hana nia ya kugombea kiti hicho.

"Nategemea Dk Slaa na viongozi wengine wa kitaifa, wakiwapo wabunge, marafiki zangu wa vyuo vikuu na wengine wengi tutakuwa nao Arumeru kuhakikisha Chadema inashinda,"alisema Nasari.

Hadi kufikia jana, kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Baraza la Vijana wa Chadema Mkoa wa Arusha (Bavicha), Ephata Nanyaro, wanachama waliokuwa wamechukua fomu ni Yohane Kimuto, Samweli Chami na Rebecca Mwingisha na leo Nasari atakuwa mwanachama wa tatu.

"Tunatarajia wanachadema wengi zaidi watajitokeza katika siku hizi zilizobaki ili kuchukuwa fomu na kurejesha mapema,"alisema Nanyaro.

Mgombea CCM alalamikia rushwa
Katika hatua nyingine, Katibu wa Uenezi na Itikadi wa CCM katika Wilaya ya Nyamagana mkoani Mwanza, Elirehema Kaaya ambaye pia ni afisa wa mifugo mkoani Mwanza, amekitaka chama hicho kukemea kampeni za fedha ndani ya chama katika uchaguzi huo.

Kaaya ambaye pia aligombea jimbo hilo katika uchaguzi uliopita na kushindwa katika kura za maoni ndani ya CCM, alisema wakazi wa Arumeru hawahitaji mgombea wa CCM ambaye anapata nafasi hiyo kwa kutumia fedha.

"Arumeru wanataka mtu wa kuwasemea matatizo yao mjengoni (bungeni) na sio mtu anayetumia fedha kupata ubunge na mimi naomba chama kikemee na kukomesha matumizi ya fedha,"alisema Kaaya.

Akizungumzia maombi hayo, Katibu wa CCM Wilaya ya Arumeru Edson Lihweuli alionya mgombea yoyote ambaye atabainika kujihusisha na vitendo vya rushwa au kukiuka taratibu atachukuliwa hatua.

Lihweuli alisema wagombea wote ambao wamechukua fomu, wamekuwa wakipewa taratibu hizo ili kuhakikisha uchaguzi ndani ya chama hicho unakwenda vizuri.

Wakati huohuo, Mkuu wa shule ya Sekondari ya Leguruki inayomilikiwa na Jumuiya ya Wazazi ya CCM, Mwalimu Athony Msami jana alijitokeza kuchukua fomu na kufanya wagombea wa chama hicho wanaomba ridhaa ya chama kufikia sita.Wengine waliokuwa wamechukuwa fomu ni Sioi Sumari, mtoto wa aliyekuwa mbunge Jeremiah Sumari, William Ndeoya Sarakikya, Elipokea Urio, Elishiria Kaaya na Elirehema Kaaya.

Wakati kada huyo wa CCM akichukua fomu, juzi jioni Mkurugenzi wa kituo cha Mikutano cha Arusha(AICC), Elishiria Kaaya alirejesha fomu na kueleza kuwa anagombea ili kutekeleza ilani kwa kushughulikia matatizo ya wananchi wa Meru.

Kaaya ambaye pia aligombea uchaguzi uliopita na kuangushwa katika kura za maoni na Marehemu Sumari, alisema miongoni mwa mambo ambayo atayasimamia ni kuhakikisha anashirikiana na wananchi kukabiliana na matatizo ya upatikanaji maji, barabara, huduma za afya na masuala ya elimu.

Takukuru yaanza kazi
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) mkoani Arusha imekutana na wagombea waliojitokeza kuchukua fomu katika uchaguzi huo na kuwaonya kutojihusisha na rushwa pia kuwataka waheshimu sheria za gharama za uchaguzi.

Takukuru pia imetamka kwamba tayari imeshashaanza kupokea malalamiko mbalimbali ya makada wa vyama tofauti vya siasa wilayani humo, kujihusisha na vitendo vya kutoa na kupokea rushwa na kwamba madai hayo yameanza kufanyiwa kazi.

Taarifa iliyotolewa na Kamanda wa Takukuru mkoani Arusha, Mbengwa Kasumambuto imesema katika kujipanga kukabiliana na rushwa katika uchaguzi huo taasisi hiyo imekutana na wagombea wote wa vyama hivyo kwa lengo la kuwatahadharisha.

“Katika kujipanga na uchaguzi wa Arumeru kwanza tumewaita wagombea ambao wameshajitokeza hadi sasa pamoja na viongozi wa vyama vyao, lengo ni kuwatahadharisha na kuwataka waheshimu sheria ya uchaguzi,”alisema Kasumambuto.


MWANANCHI